Showing posts with label Urembo na fasheni. Show all posts
Showing posts with label Urembo na fasheni. Show all posts

Tuesday, December 5, 2017

Madhara ya Kujichubua

12/05/2017 09:28:00 AM 0

Madhara ya kujichubua

Urembo na kuwa na ngozi yenye mvuto  ni kitu ambacho karibia kila mtu anapenda. Siku hizi imekuwa kawaida kukutana na mtu akiwa kajipendezesha hasa uso. Hii ni kwasababu wengi tunaamini uso ndio kitu cha kwanza kuonwa na watu yaani face is introduction for everyone 


Katika baadhi ya sehemu duniani watu wanaamini kuwa ngozi angavu huashiria uzuri, utajiri na uwezo(kifedha) alionao mtu. Katika baadhi ya sehemu watu wenye ngozi nyeusi huchukuliwa kuwa wapo chini ya kiwango, hii hupelekea watu hawa kutumia ving´arisha ngozi kama krimu, vidonge au nyenzo zingine kubadilisha ngozi zao. Idadi inazidi kukua maradufu ya matumizi ya ving'arisha ngozi, na siku hizi hata wanaume wapo tofauti na zama za kale ambapo mabinti walishika usukuni.

 Tafiti zinaonyesha kwamba wavulana na wasichana hupendelea kutumia bidhaa zinazong´arisha ngozi ili waweze kupata hadhi nzuri katika kundi la familia zao, na jamii. Kwa kweli,hata matangazo yanayoonyeshwa kwenye televisheni mbalimbali huonyesha kitu hiki.

Mambo hayo yote huwa na athari kubwa juu ya mawazo ya vijana wa kiume na wakike ambayo hupelekea kuwafanya wachague chochote wanachomudu kati ya krimu au vidonge.

Je kuna madhara kujichubua...?

  • Jibu ni rahisi tu, ndiyo yapo tena sana kama sio leo basi kesho kwa wewe unayetumia! Nimekuandikia hapa madhara yasome uelewe mtu wangu..u anaeyejichubua anaweza kupata kansa ya ngozi, chunusi, uvimbe katika ngozi, ngozi kuwa nyembamba na kukosa uimara katika uvutikaji yaani stretiching ambapo mtu huyu akipata ajali sio rahisi kushona kwa kuwa ngozi hukatika tu! 
  • Kuongezeka kwa hamu ya kula na uzito, wengi wameongezeka uzito bila kujijua hii inatokana na baadhi ya krimu ama vidonge kuongeza hamu ya kula
  • Kutokwa na mabaka na mavipele makubwa ambayo siyo rahisi kupona na hufanya mtu akose mvuto na raha, wapo wengi wako katika hali hii. U
  • Ugonjwa wa pumu kutoka na krimu ama vidonge kuathiri mapafu na mfumo wa upumuaji. K
  • Kupata watoto wenye kasoro baadhi ya madini na viambata vilivyopo kwenye ving'arisha ngozi huathiri mbegu na mfumo wa uzazi hivyo kuathiri aina ya watoto mtu atako zaou
  • Kupata matatizo ya akili na kuharibika kwa ini, ini huaribika kutokana na kushindwa kukabili sumu ya dawa ambazo mtu katumia. K
  • Kuharibika kwa mishipa ya fahamu pamoja na figo kutokana na kiwango kikubwa cha zebaki(mercury) kilichomo katika krimu, Osteoporosis(kupungua kwa uzito wa mifupa ambapo huongeza hatari ya kuvunjika kwa mifupa)

Kuungua kwa uso na kubaki na ngozi yenye makovu makovu na isiyovutia.. 
Baadhi ya madhara haya huonekaa mara moja na mengine hujitokeza kadri mtu anavyotumia ving´arisha ngozi na kadiri anavyozidi kuzeeka. 
Waweza kupendeza leo ila ukawa unajichimbia kaburi la mateso hapo baadae, kumbuka fainali uzeeni na siku zote kujikubali ulivyo ndio silaha ya kwanza. 
Waweza kushare maarifa haya kuokoa wengine



Rudisha mvuto wa ngozi kwa Njia asilia

12/05/2017 09:08:00 AM 0
Njia za asili za Kuondoa mikunjo ya ngozi
MIKUNJO katika ngozi ni miongoni mwa matatizo yanayowakabili wanawake wengi.

Tofauti na mikunjo ya uzee, mikunjo hii hutokana na kuchoka kwa ngozi kunakosababishwa na mambo mablimbali ikiwemo matumizi ya vipodozi vyenye kemikali kali ambayo huondoa uhalisia wa ngozi.
Katika kupambana na tatizo hilo, wadau wa urembo wa asili wamegundua njia mbalimbali zinazoweza kutumika kutatua tatizo hili.
Wadau hao wanashauri kumwona mtaalamu wa afya kwa ushauri zaidi wa matumizi ya njia hizo za asili kabla ya kuanza kutumia njia za asili kwani hata kama ni vipodozi asilia, haina maana kama ni salama kwa watu wote.
Kwa mujibu wa wadau hao, unaweza kutumia viungo vinavyopatikana jikoni kwako kupambana na mikunjo katika ngozi. Baadhi ya viungo hivyo ni pamoja na:
Karoti
Tumia juisi ya karoti kwa kupaka katika ngozi yako, hasa katika maeneo yaliyoathirika.
Karoti ina virutubisho muhimu kwa ngozi yako. Pia ina uwezo mkubwa wa kuondoa sumu ndani ya ngozi.
Si hivyo tu, karoti inaweza kuondoa kabisa tatizo la mikunjo ya
ngozi hasa sehemu za pembeni ya macho, shingo na maeneo kama hayo.
Jinsi ya kuandaa na kutumia.
Chukua karoti, saga kwenye mashine kisha kamua ili kupata juisi yake.
Tumia pamba kupaka katika maeneo yaliyoathirika, fanya hivyo mara kwa mara, itakusaidia kupunguza ama kuondoa kabisa tatizo hilo.
Maziwa
Maziwa yana virutubisho vinavyochochea kunawiri kwa ngozi.  Pia yana chembechembe za 'Alfa-Hydroxide Acid' ambazo zina uwezo mkubwa kuondoa seli zilizokufa mwilini.
Yote haya husaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa tatizo la mikunjo katika ngozi.
Unachotakiwa kufanya
Kuchukua maziwa kiasi na chovya pamba ndani yake, kisha paka maeneo yaliyoathirika.
Aloe Vera
Jeli ya Alovera ndiyo hasa inayotakiwa katika zoezi hili. Chukua jani lake na kisha likate ili kupata utomvu wake.
Chukua utomvu au jeli hiyo kama wengine wanavyoita na kisha pakaa sehemu iliyoathirika, itapunguza ama kuondoa kabisa tatizo hilo.
Parachichi
 'Mask' ya Parachichi husaidia kuifanya ngozi iwe na mng'ao. Siyo hivyo tu, bali huchangia kwa kiasi kikubwa pia kuifanya ngozi iwe laini na nyororo.
Jinsi ya kutayarisha na kutumia
Chukua parachichi liloiva vizuri, kisha saga hadi lilainike.
Baada ya hapo pakaa sehemu iliyoathirika na acha kwa muda wa dakika 10, kisha osha sehemu hiyo uikaushe.

Papai
Mask ya Papai pia husaidia kuondoa tatizo hili.
Unachotakiwa kufanya...
Chukua kipande cha papai kilichoiva na kuchanganya na kijiko kimoja cha unga wa ngano.
Pakaa sehemu iliyoathirika na kaa nayo kwa muda usiopungua dakika kumi. Mbali na kupaka pia unaweza ukatumia kula kwani lina vitamin E kwa wingi, ambavyo ni muhimu katika ukuaji wa ngozi.
Danzi
Juisi ya tunda hili husaidia katika uzalishaji wa sehemu ya juu ya ngozi 'collagen'. Danzi lina kiwango kikubwa cha vitamini C.  Na kwa kawaida aina hii ya vitamin husaidia kuchochea ukuaji wa ‘collagen’, hivyo kuifanya ngozi yako kunawiri.
Maji
Kunywa maji mengi kwani husaidia kuifanya ngozi yako iwe na unyevu muda wote.
Ikiwa utazingatia zoezi hili mikunjo kati ngozi yako itakuwa ni historia.

Audio