Tuesday, November 21, 2017

Kwanini Wapenzi Wanaachana?

KUACHANA NA MPENZI WAKO AU MCHUMBA

Kuvunjika kwa uhusiano au kusalitiana baina ya wapendanao kimekuwa kitu cha kawaida sana siku hizi. Angalabu zaid ya asilimia 95% ya vijana wamekumbwa au walishawahi kukumbwa na kisanga hiki. Kiufupi kusaliatiana au kuacha katika uhusiano ni jambo baya sana kwa kuwa hakuna mtu mjinga anaye anzisha mahusiano  na mtu pasi  na malengo.

Vijana wengi kwa sasa wanaumwa ugonjwa kitaalamu  unaitwa “LOVE CONCUSION” yaani kutokana na kusalitiwa basi wanaogopa sana kuwa na mahusiano ama hawawi na imani tena pindi wawapo na mahusiano kwa mara nyingine.  Hili ni tatizo kubwa sana na linahitaji muda kulijadili…

TATIZO LIKO WAPI? KIPI KINSABABISHA?
Kuna mambo mengi  sana yanayosabababisha uhusiano wa wapendanao kuvunjika. Leo mwalimu wako nitakufunza machache ili udumishe uhusiano wako na kama basi yamekukuta uone namna gani ya kuishi upya ukirekebisha pale ulipo kosea…karibu…

1: AHADI, katika mahusiano  ahadi hutawala sana, mara nitakununulia gari, mara nyumba kimala mara masaki. Mara nitakuoa, au lazima niolewe na wewe! Hatukatai ila angalia kabala ya kutamka utaweza kutekeleza? Pia kuna kipindi ambapo watu hulewa sana mapenzi na kujikuta unatoa ahadi usizoweza hasa wanaume..mwisho wa siku yanakushinda unajikuta unaliaa…NOTE “KAMWE USITOE AHADI UKIWA NA FURAHA SANA” kwa kuwa utaongea hata usivo weza kutekeleza. Toa ahadi ukiwa katika hali ya kawaida mno..

2: Aina ya mahusiano na Umri: katika vitu vinavyo umiza ni pamoja na kuwa na uahusiano na mtu katika umri ambao bado akili haija pevuka. Yaani bado hujabalehe kisawasawa ukajua kutofautisha kati ya kupenda na tamaa na hisia za mwili. Unakuta mtu alimpenda mtu wakiwa wadogo mno maybe miaka 16 wakikua na kufika 23 anaona vizuri zaidi mwisho ana achana na mchumba wake ambaye wametoka  naye mbali, umri sahihi kwa mwanaume kutulia na kuanzia22  so usione kwanini wanaachana kozi umri ni tatizo. Kama hujakua vizuri acha hizo, wazuri wapo na mahendsome wapo, unawahi nini?

3: Kipi kilikuvutia na mlianzishaje Mahusiano: unakuta watu wakati wanaanza walikuwa wanapendana sana simu kila dakika, kutembeleana kila mara, wameshikana mikono kama kumbikumbi, leo usipomshika mkono lazima ajiulize kwanini? Usipopokea simu lazima ajiulize kwann? Usipotembea nae barabarani lazima ajiulize kwanini? So usiigize tabia kuwa wewe ni mwema sana, onesha tabia yako halisi ili mtu akujue mapema, kuigiza tabia mpka lini?, ndio hapo mwisho mtu akigundua anakuacha. Ulipendelea kuhonga sana endelea kuhonga si ulimdekeza kama hutatoa jua wengine watahonga maana ndio ulimdekeza hivo…

4: Umbali na mpenzi wako: hapa ndio penye tatazo kwa macho yakinifu, uko Mwanza jamaa yuko huko Peramiho Songea. Siwakatishi tamaa ila kuna mtu alishwahi sema “ni Waafrika wachache  sana wanaweza Far love” yaani mapenzi yambali. Kwahiyo kama unataka kuoa hakikisha upo karibu na mpenzi waka au kama upo mbali basi mtembelee kila mara laasivyo ujue tu mambo yataharibika. Ukikaa na mtu karibu kwa mda mrefu hata km ni rafiki tu unajikuta kuna upendo flani ambao mwisho wa siku unaleta mapenzi kabisa so akiwa mbali ndio hivyo tena. Muombe Mungu mwema na kuwa na imani nae hakika subra ndiyo ushindi..  

5: Matumizi ya Simu na Mitandao ya kijamii: hapa pameleta kiza zaa kwa watu wengi. Je huwa unaichunguza simu ya mpenzi au mchumba wako? Je unafuatilia post maybe insta, wasap, fb nk? Kma jibu ni ndiyo  basi upo hatarini na kama jibu ni hapana  basi uko salama ila SI SALIMINI! Simu zinadanganya sana watu, yaani unaongea nae saa 2 anakwambia “bebi nimchoka nalala mwaa”! Nenda fb online, wasap online, insta ndio anapest saa 7 usiku, hilo jipu jua tu yupo ANAYE MUWEKA ONLINE ndio maana akakwambia  analala. Usijidanganye, simaanishi ukavuruge uhusiano kwa kuwa online mpaka saa 8 ila kuwa makini, hata mbuyu ulianza kama mchicha…..

6: Tabia za kuiga, wengi sana wanalia baada ya kuachana na wapenzi waliowapenda kwa dhati kisa wameiga na kujikuta katika hali ngumu. Kwanini uige kisa Fulani kasema hiki au kafanya hiki? Kuwa na wapenzi wangi sio kitu na wala sio ustaarabu kabisa, sasa utasikia nakuwaje nae mmoja akiniacha je?  hapo mimi pia sina jibu ila tuache kuiga tabia fulani zitakazo pelekea kuvunjika uhusiano, unakuta mtu alipendwa akiwa na kipara na anavaa nguo za kawaida, baada ya muda mara sijui vimini mara visuruali vya ajabu ajabu, kama mtu hakukuta katika hayo na hapendi basi acha, usiige fasheni itakuachanisha na mtu wa muhimukwako…

7: Kupenda vya Mteremko, hapa wanaume wengi imewaumiza sana kwa kuachwa, kwa kuwa hawaa pesa na unakuta binti alie nae anataka vitu vya bei ila tambua penzi la kweli latoka moyoni si pesa. Kwa kuwa mvulana hana basi atasemwa kila neno mwisho ATAKA TAMAA. Ewe binti, mwanaume bora ni Yule uanyeanza nae AKIWA HANA KITU. Hao wenye  pesa watakutumia tu wakuache kama TAMABARA bovu lisiliafaa hata kwa kudekia. Leo hii unamwacha mchumba anayekupenda kisa mwanaume mwenye pesa utaolewa kama mke wa tatu jidanganye, endelea kujidanganya utajuta sana. Mwanume hangaika utafanikiwa na anayekukacha kisa masikini muombee heri tu aendako…ila akirudi utajua wewe umsamehe au laa!!!!!!!!!!!!!!

Mwisho, kuvunjika kwa uhusianao ama kuachana ni kitu kibaya sana, tumeshudia watu wakijiua, wakiwa machizi na wakfeli mitahani na kuwa na vusasi moyoni ! Kwanni turudishane nyuma kwa tamaa tu? Ewe binti, ewe kijna hakuna mpenzi  bora ZIDI YA HUYO ULIYE NAYE, hebu vumilia na utaona raha. Kma unapendwa pendeke na kama UMESALITIWA POLE. Dunia siyo mbaya walimwengu ni wabaya. Na ewe binti au kijana unayeharibu mahusiano ya wengine  basi jua kuwa ipo siku tu na wewe utapenda na Yule uliempenda atatwaliwa na wengine. 
Tukumbuke Kumshrikisha Mungu kwakuwa kila chema kimeumbwa na yeye. Pia ni mhimu mno kuwa karibu na mpenzi wako mkawa mnasali pamoja na kumuomba Mungu awasaidie ili baadae muwe baba na mama….

Pole kwa wale wenye maumivu na makovu ya kuvunjika kwa uhusiano, usijali mwingine  yupo kwaajili yako ….

Well said
#want_see_you_change_everyday
Franco Samuel

No comments:

Post a Comment

Audio